Wednesday 7 September 2016

Abduba Dida ataweza kuwania urais tena 2017?

Aliyekuwa katika kinyang’anyiro cha ugombea urais wa mwaka 2013  Mohammed Abduba Dida amejitokeza kwa mara nyingine na kutangaza azma yake ya kutaka kuwania tena  kiti hicho
Abduba Dida ataweza kuwania urais tena 2017?
Dida alisema kuwa yuko katika jitihada za kuunda muungano mpya utakaowahusisha viongozi kutoka katika vyama mbali mbali.

Imesemekana kuwa Dida tayari amekutana na baadhi ya viongozi hao wakiwemo Musalia Mudavadi, Peter Kenneth, Martha Karua, Paul Muite na katibu mkuu wa chama cha waalimu (KNUT), Bw. Wilson Sossion.
Abduba Dida ataweza kuwania urais tena 2017?
Aidha, Dida pia alikutana na aliyekuwa  waziri na mgombea mwenza katika uchaguzi wa 2013, James Ole Kiyapi na mwanasheria Ekuru Aukot.
Dida vile vile aliwataja  Maryam Sheikh, Amina Guyo na Esther Ali Ibrahim kama walio na uwezo wa kuungana naye 2017

No comments:

Post a Comment